UONGOZI NI MSINGI WA MAENDELEO..... #InsideStoryBook2020: LADDER OF LEADERSHIP FOR THE NEXT GENERATION LEADERS: 10 Steps to Enrich Your Leadership Potential

“Uongozi ni msingi au sharti kuu la maendeleo endelevu kwa nchi yeyote ile” Prof. Joseph Semboja Wanazuoni wa Sayansi ya Siasa na Uchumi Prof. Daron A. na Prof. J. Robnson katika Kitabu chao Why Nations Fail: The Origin of Power, Poverty and Prosperity wamefanya uchambuzi linganifu wa maendeleo baina ya nchi mbalimbali duniani. Matokeo ya utafiti wao kuhusu utofauti wa kiwango cha maendeleo kati ya nchi hizo, yanaeleza chanzo cha umasikini na utofauti wa kiwango cha maendeleo ni kutokana na taasisi zilizopo katika nchi husika, kwa maana ya taasisi za kisiasa, kiuchumi na kijamii. Nchi zenye taasisi imara (strong institutions) zina kiwango kikubwa cha maendeleo ukilinganisha na nchi zenye taasisi dhaifu (weak institutions). Taasisi imara ndiyo kichocheo cha maendeleo endelevu na taasisi dhaifu ni kikwazo cha maendeleo. Taasisi hizi hazijitengenezi zenyewe bali zinajengwa na kuimarishwa na #VIONGOZI. Uongozi una determine aina ya taasisi za nchi husika. Mathalani nchi za Asia (Four...